Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Wizara ya Kilimo

Bw. Gerald G.Mweli

Bw. Gerald G.Mweli
Katibu Mkuu

Dkt. Stephen J. Nindi

Dkt. Stephen J. Nindi
Naibu Katibu Mkuu (Ushirika na Umwagiliaji)

Dkt. Hussein M. Omar

Dkt. Hussein M. Omar
Naibu Katibu Mkuu (Maendeleo ya Mazao na Usalama wa Chakula)

Slide Photo
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo anayeshughulikia Umwagiliaji na Ushirika, Dkt. Stephen Nindi akizungumza katika kikao cha menejimenti ya Tume ya Taifa ya Umwagiliaji. Kikao hicho kimefanyika Mei 9, 2025 katika Ofisi za Tume ya Taifa ya Umwagiliaji jijini Dodoma.
Slide Photo
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo anayeshughulikia Umwagiliaji na Ushirika, Dkt. Stephen Nindi akiipongeza Tume ya Taifa ya Umwagiliaji kwa juhudi inazofanya katika utekelezaji Miradi mbalimbali ya Umwagiliaji nchini. Dkt. Nindi ametoa pongezi hizo leo Ijumaa Mei 9, 2025 alipotembelea Ofisi za Tume ya Taifa ya Umwagiliaji jijini Dodoma na kufanya kikao na menejimenti ya Tume na kuwasihi kuendelea na jitihada wanazofanya katika kuboresha sekta ya Kilimo cha Umwagiliaji kwani nchi ina maeneo makubwa yanayofaa kwa Kilimo cha Umwagiliaji.
Slide Photo
Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Bw. Gerald Mweli akizungumza katika hafla ya kupokea Cheti cha Ithibati na Ubora wa Kimataifa wa Maabara ya Udongo na Mimea ya Taasisi ya Utafiti wa Chai Tanzania (TRIT) yenye ithibati namba ( ISO/ICE 17025:2017) tarehe 9 Mei, 2025 jijini Dodoma.
Slide Photo
Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Bw. Gerald Mweli akiwa katika hafla ya kupokea Cheti cha Ithibati na Ubora wa Kimataifa wa Maabara ya Udongo na Mimea ya Taasisi ya Utafiti wa Chai Tanzania (TRIT) yenye ithibati namba ( ISO/ICE 17025:2017) tarehe 9 Mei, 2025 jijini Dodoma.
Slide Photo
Makabidhiano rasmi ya vituo vya kukusanyia mazao ya Horticulture kwa viongozi wa vikundi vya wakulima wa maeneo mbalimbali kutoka Wilaya za Waning’ombe na Njombe. Makabidhiano hayo yamefanyika katika viwanja vya Itulike Aman katika hafla ya uzinduzi wa vituo hivyo tarehe 8 Mei 2025. Hafla hiyo pia ameshiriki Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo anayesimamia Maendeleo ya Mazao na Usalama wa Chakula, Dkt. Hussein Mohamed Omar (aliyemwakilisha Katibu Mkuu Bw. Gerald Mweli); na viongozi wengine akiwemo Mgeni Rasmi, Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Anthony Mtaka.
Slide Photo
Slide Photo
Slide Photo
Afisa Mtendaji Mkuu wa TAHA, Dkt. Jacqueline Mkindi akikabidhi zawadi kwa Mgeni wa Heshima Naibu Katibu wa Wizara ya Kilimo anayesimamia Maendeleo ya Mazao na Usalama wa Chakula, Dkt. Hussein Mohamed Omar (aliyemwakilisha Katibu Mkuu Bw. Gerald Mweli); na viongozi wengine akiwemo Mgeni Rasmi, Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Anthony Mtaka kama ishara ya shukurani na kuendelea kuonesha ushirikiano kati ya TAHA na Serikali, ikiwa pia ni muendelezo wa kusherehekea miaka 20 tangu kuanzishwa kwa TAHA.
Slide Photo
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo anayesimamia Maendeleo ya Mazao na Usalama wa Chakula, Dkt. Hussein Mohamed Omar amesema kuwa Vituo vya Kukusanyia Mazao ya Horticulture vinaendana kuwa suluhisho kwa wakulima wa parachichi katika kupata huduma za usimamizi wa ubora, uhifadhi wa muda mfupi na maandalizi ya usafirishaji wa mazao yao kwenda sokoni, hasa masoko ya nje. Amesema hayo tarehe 8 Mei 2025 Mkoani Njombe ikiwa ni sehemu ya kusheherekea Miaka 20 ya Taasisi ya Wakulima wa Mbogamboga na Matunda (TAHA), na kuongeza kuwa vituo vitasaidia kupunguza upotevu wa mazao, kuboresha ubora, na kuongeza thamani ya bidhaa katika masoko ya Kimataifa.
Slide Photo
Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussen Bashe (Mb) katika picha akiwa ni miongoni mwa Viongozi wa Serikali walioshiriki katika hafla ya tuzo zinazoitwa “Samia Kalamu Award”, kwenye Ukumbi wa Super Dome Masaki, jijini Dar es Salaam tarehe 05 Mei 2025. Mhe. Bashe pia alipata muda wa kuongea na Kaimu Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Mhe. Andrew Lentz. Mgeni Rasmi katika hafla ya utoaji wa tuzo hizo ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan.